Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ofisi ya Msajili: Mkapa ana historia ndani ya CUF
Habari za Siasa

Ofisi ya Msajili: Mkapa ana historia ndani ya CUF

Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania
Spread the love

SISTY Nyahoza, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania amesema, Hayati Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya tatu ameacha mchango wake ndani ya Chama cha Wananchi (CUF). Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho ulioitishwa kwa ajili ya kupitisha majina ya wagombea urais Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar leo Jumatatu tarehe 27 Julai 2020, Nyahoza amesema, miongoni mwa mambo aliyoanzisha Rais mstaafu Mkapa yaliinufaisha CUF.

Amesema, mwaka 1995, Rais Mkapa alianzisha ruzuku ya chama na kwamba, miongoni mwa vyama vya mwanzo kunufaika na ruzuku hiyo ni CUF.

“CUF ilianza kunufaika na mpango wa Rais Mkapa, lakini tulikuwa na tatizo la siasa Zanzibar, Rais Mkapa ndiye aliyesimamia na kutatua mgogoro huo kwa kusaini mkataba wa marudhiano. Sio hivyo tu, Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar uiliratibiwa na Rais Mkapa ndio maana nasema Mkapa ana historian a CUF,” amesema.

Pia, Nyahoza amesema, mpango wa Viti Maalum mwaka 2005 ulionzishwa na Rais Mkapa, CUF ni miongoni mwa vyama vya mwanzo vilivyonufaika.

Msajili huyo pia ameipongeza CUF kwa dhamira ya kufanya siasa za kistaarabu katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

“Naipongeza CUF kwa kuamua kusimamia kauli ya kufanya kampeni kwa ustaarabu. Ninaamini mtasimamia kauli hiyo, lakini pia nampongeza Prof. Lipumba kwa kuandaa mkutano huu,” amesema Nyahoza na kuongeza “CUF bado ipo imara.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!