Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ofisa Chadema apigwa risasi, auawa
Habari za Siasa

Ofisa Chadema apigwa risasi, auawa

Spread the love

LUCAS Lihambalimu, Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Jimbo la Malinyi mkoani Morogoro jana usiku tarehe 12 Juni 2019, amepigwa risasi nyumbani kwake na kuuawa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).  

Tumaini Makene, Msemaji wa Chadema kwenye taarifa yake amesema, Lihambalimu ameuawa akiwa nyumbani kwake.

Ameeleza kuwa, Lihambalimu alivamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake maeneo ya Bonde la Kilombero saa nane usiku, ambao walimpiga risasi na kupoteza maisha yake.

 “Watu wenye silaha walifika nyumbani kwa Lihambalimu , wakagonga wakamtaka atoke nje wanasgida naye. Akiwa wanatafuta upenyo wa kuchungulia kuwajua ni wakina nani, walimfyatulia risasi kichwani na kumuua hapo hapo,” imeeleza taarifa ya Makene.

 MwanaHALISI ONLINE ilimtafuta Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro kwa njia ya simu kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa tukio hilo, hata hivyo amesema, hana taarifa hizo kwa kuwa, yupo nje ya ofisi kutokana na matatizo ya kiafya.

Kamanda Mutafungwa aliahidi kutoa mawasiliano ya msaidizi wake, kwa ajili ya kueleza undani wa tukio hilo, lakini hadi taarifa hili inachapishwa hakutuma namba za msaidizi wake.

“Bahati mbaya mimi ni mgonjwa, niko hospitali napata matibabu, nahangaika na huduma za kiafya. Nitakupa namba za msaidizi wangu ambaye utamhoji na kuendelea naye kwa taratibu za kiofisi,” amesema Kamanda Mutafungwa.

Hata hivyo Makene amesema, Chadema inafuatilia kwa karibu kifo hicho “Tunafuatilia taarifa mbaya kuhusu K/Mwenezi, Jimbo la Malinyi, Morogoro, Lucas Lihambalimu aliyevamiwa nyumbani kwake, kupigwa risasi na kufariki hapohapo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!