Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Odinga na Kenyatta waahidi amani
Makala & UchambuziTangulizi

Odinga na Kenyatta waahidi amani

Uhuru Kenyatta (kulia) na Raila Odinga
Spread the love

WAGOMBEA wa urais wawili wenye nguvu nchini Kenya, Raila Odinga (NASA) na Uhuru Kenyatta (Jubilee), leo wamepiga kura katika uchaguzi mkuu nchini humo huku kila mmoja akisisitiza suala la kulinda amani, anaandika Mwandishi Wetu.

Kenyatta amepiga kura katika eneo lao la asili alipozaliwa la Gatundu na Odinga alikwenda na kupiga kura katika eneo la Kibera.

Misululu ya wananchi wa Kenya imeonekana leo nchini humo, lakini wananchi katika maeneo mbalimbali wakionekana watulivu na wanaofuata utaratibu.

Inaelezwa kuwa kuna baadhi ya maeneo yanakabiliwa na mvua na kusababisha usafiri kuwa mgumu katika sehemu hizo.

Hata hivyo imeripotiwa kuwa katika maeneo ya Embakasi kulikuwa na ucheleweshaji wa kuanza kupiga kura.

Wapigakura milioni 20 nchini humo wanatarajia kupiga kura katika uchaguzi huo ambao unaonekana kuwashindanisha vigogo hao wawili Odinga na Kenyatta.

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

Habari za SiasaTangulizi

ACT Wazalendo washtushwa vifo 47 mafuriko Hanang

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeelezza kupokea kwa mshtuko na simanzi...

error: Content is protected !!