Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Odinga na Kenyatta waahidi amani
Makala & UchambuziTangulizi

Odinga na Kenyatta waahidi amani

Uhuru Kenyatta (kulia) na Raila Odinga
Spread the love

WAGOMBEA wa urais wawili wenye nguvu nchini Kenya, Raila Odinga (NASA) na Uhuru Kenyatta (Jubilee), leo wamepiga kura katika uchaguzi mkuu nchini humo huku kila mmoja akisisitiza suala la kulinda amani, anaandika Mwandishi Wetu.

Kenyatta amepiga kura katika eneo lao la asili alipozaliwa la Gatundu na Odinga alikwenda na kupiga kura katika eneo la Kibera.

Misululu ya wananchi wa Kenya imeonekana leo nchini humo, lakini wananchi katika maeneo mbalimbali wakionekana watulivu na wanaofuata utaratibu.

Inaelezwa kuwa kuna baadhi ya maeneo yanakabiliwa na mvua na kusababisha usafiri kuwa mgumu katika sehemu hizo.

Hata hivyo imeripotiwa kuwa katika maeneo ya Embakasi kulikuwa na ucheleweshaji wa kuanza kupiga kura.

Wapigakura milioni 20 nchini humo wanatarajia kupiga kura katika uchaguzi huo ambao unaonekana kuwashindanisha vigogo hao wawili Odinga na Kenyatta.

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!