Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Odinga apimwa COVID-19, alazwa hospitalini
Kimataifa

Odinga apimwa COVID-19, alazwa hospitalini

Raila Odinga
Spread the love

 

RAILA Odinga, kiongozi wa chama cha upinzani cha ODM, amefikishwa katika Hospitali ya Nairobi, Kenya na kuchukuliwa vipimo vya corona (COVID-19). Umeeleza mtandao wa The Standard Kenya … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na kaka yake, Oburu Odinga leo Jumatano tarehe 10 Machi 2021, kwamba kiongozi huyo wa upinzani amekwenda hospitali hiyo leo asubuhi.

“Odinga amechukuliwa vipimo vya COVID-19, lakini mpaka sasa majibu yake hayajatoka,” amesema Oburu na kuongeza “amekuwa akilalamika uchovu na maumivu.”

Oburu amesema, mdogo wake alieleza kulalamikia maumivu ambapo aliamua kusitisha ziara yake ya Pwani, alipokua katika eneo la Karen.

Mara baada ya kuchukuliwa vipimo hivyo, kiongozi huyo wa upinzani, hakuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!