MGOMBEA urais nchini Kenya kupitia muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga jana Agosti 14, 2022 ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza tangu siku ya uchaguzi tarehe 9 Agosti na kutoa ujumbe wa kudumisha amani kwa raia wa taifa hilo la Afrika Mashariki. Anaripoti Mwandishi … (endelea).
Jana Jumapili Odinga amehudhuria ibada katika kanisa la Mtakatifu Francis ACK lililopo huko Karen jijini Nairobi huku akiwa ameambatana na Mgombea mwenza, Martha Karua.
Pia Odinga aliambatana na viongozi wa chama chake ODM pamoja na washirika wake akiwamo Mwenyekiti wa Kanu, Gideon Moi na Mbunge mteule wa Lang’ata, Phelix Kodhe.
Akiwa kanisani Raila alinukuu Sala ya Mtakatifu Francis Asizi inayosema,”Bwana, utufanyie vyombo vya amani yako. Palipo na chuki na tupande upendo; penye madhara, msamaha; penye ugomvi, umoja….”
Pamoja na sala hiyo Odinga alisema anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumvusha salama katia kipindi cha kampeni n ahata zoezi la upigaji kura.
“Huko kote kulikuwa na changamoto lakini tumevuka kwa amani ni matumaini yangu kwamba amani itaendelea kutawala taifa letu hata baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa kwa sababu sisi ni sehemu ya taifa hili na Kenya itaendelea kuwa imara hata baada ya uchaguzi,” amesema.
Alisema yeye ni Mkenya hivyo anatamani kuona amani, umoja na upendo vikiendelea kutawala taifa hilo.
Leave a comment