RAIS Barrack Obama anayemaliza muda wake wa kukaa Ikulu ya Marekani siku ya kesho amepuuza msimamo wa chama chake cha Democtatic kususia sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule Donald Trump, anaandika Wolfram Mwalongo.
Obama amesema atashiriki kikamilifu zoezi la kumkabidhi madaraka Trump licha ya msimamo wa chama chake wa kususia tukio hilo la kihistoria.
Akizungumza katika mkutano wake wa kuagana na wanahabari aliofanya nao kazi kwa miaka nane, Obama amesema Wamarekai hawapaswi kuwa na hofu kwani Taifa hilo ni la Wamarekani wote.
“Nina imani na nchi yangu na watu wake,” amesema Obama.
Obama ameeleza kuwa kitu alichomshauri Trump ni kushirikiana na wasaidizi wake kwani kazi ya Urais ni kubwa na ngumu.
“Hii ni kazi yenye maana kubwa, hawezi kuifanya peke yake nimeshauri kuwa ni lazima ashirikiane na wasaidizi wake,” amesema.
Ametumia nafasi hiyo kuitakia heri familia ya George W. Bush Rais wa 41 wa Marekani ambaye amelazwa hospitali pamoja na mkewe Barbara kutokana na matatizo ya kiafya.
Obama pia amedai bado anaamini kuwa upo uwezekano mkubwa Marekani ikaongozwa na rais Mwanamke siku zijazo huku akisema Wamarekani wenye asili ya kigeni waendelea kujitokeza kwenye vinyang’anyiro vya nafasi mbalimbali bila kuhofia chochote.
“Natarajia kuona ongezeko la Wamarekani wenye asili ya mataifa ya kigeni wakiongezeka katika vinyang’anyiro vingi katika pembe zote za Marekani na huenda tukapata rais Mwanamke kutoka huko,” amesema Obama.
Leave a comment