Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Obama akipuuza chama chake
Kimataifa

Obama akipuuza chama chake

Barack Obama, Rais wa Marekani anayemaliza muda wake
Spread the love

RAIS Barrack Obama anayemaliza muda wake wa kukaa Ikulu ya Marekani siku ya kesho amepuuza msimamo wa chama chake cha Democtatic  kususia sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule Donald Trump, anaandika Wolfram Mwalongo.

Obama amesema atashiriki kikamilifu zoezi la kumkabidhi madaraka Trump licha ya msimamo wa chama chake wa kususia tukio hilo la kihistoria.

Akizungumza katika mkutano wake wa kuagana na wanahabari aliofanya nao kazi kwa miaka nane, Obama amesema Wamarekai hawapaswi kuwa na hofu kwani Taifa hilo ni la Wamarekani wote.

“Nina imani na nchi yangu na watu wake,” amesema Obama.

Obama ameeleza kuwa kitu alichomshauri Trump ni kushirikiana na wasaidizi wake kwani kazi ya Urais ni kubwa na ngumu.

“Hii ni kazi yenye maana kubwa, hawezi kuifanya peke yake nimeshauri kuwa ni lazima ashirikiane na wasaidizi wake,” amesema.

Ametumia nafasi hiyo kuitakia heri familia ya George W. Bush Rais wa 41 wa Marekani ambaye amelazwa hospitali pamoja na mkewe Barbara kutokana na matatizo ya kiafya.

Obama pia amedai bado anaamini kuwa upo uwezekano mkubwa Marekani ikaongozwa na rais Mwanamke siku zijazo huku akisema Wamarekani wenye asili ya kigeni waendelea kujitokeza kwenye vinyang’anyiro vya nafasi mbalimbali bila kuhofia chochote.

“Natarajia kuona ongezeko la Wamarekani wenye asili ya mataifa ya kigeni wakiongezeka katika vinyang’anyiro vingi katika pembe zote za Marekani na huenda tukapata rais Mwanamke kutoka huko,” amesema Obama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

error: Content is protected !!