Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Nyumba ya mchezaji wa Simba kupigwa mnada
Michezo

Nyumba ya mchezaji wa Simba kupigwa mnada

Emmanuel Gabriel
Spread the love

 

KAMPUNI ya udalali ya Greenlight kwa idhini ya Mahakama ya Mwanzo ya Wilaya ya Kinondoni kituo cha Ukonga, jijini Dar es Salaam, itaiuza nyumba ya mchezaji wa zamani wa Simba, Emmanuel Gabriel Mwakyusa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Nyumba hiyo ya mshambuliaji huyo wa Simba ipo Kitunda jijini humo, itauzwa tarehe 22 Oktoba 2021 kuanzia saa 8:00 mchana.

Ni baada ya Anna Abeid Salum, kushinda madai namba 91/2018 mahakamani hapo.

Tangazo kwa umma lililotolewa leo Jumatano, tarehe 13 Oktoba 2021 na kampuni hiyo ya udalali inaeleza masharti yatakayotumika bila kuathili masharti yaliyopo katika tamko la kuuza.

“Wanunuzi wote watatakiwa kuzingatia vigezo na masharti watakayopatiwa na dalali wa mahakama wakati wa mnada. Ukaguzi wa mali unaruhusiwa kuanzia tarehe ya tangazo kutoka,” linaeleza tangazo hilo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!