Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Nyuklia yazidi kumtesa Rais Trump 
Kimataifa

Nyuklia yazidi kumtesa Rais Trump 

Spread the love

RAIS wa Marekani Donald Trump amesaini sheria mpya ya kuongeza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini juu ya mpango wake wa zana za Nyuklia kwa madi kwamba ni hatarishi kwa usalama wa taifa lake, anaandika Catherine Kayombo.

Kupitia Waziri wa Fedha wa Marekani, Trump ameidhinisha vikwazo hivyo  dhidi ya makampuni ya fedha yanayofanya biashara zake ndani ya Korea Kaskazini.

Ikiwa ni njia mojawapo ya kuyumbisha uchumi wa nchi hiyo katika biashara yake ya Nyuklia, rais wa Marekani amesema kuwa benki kuu ya China imeagiza taasisi za fedha kuacha kufanya biashara na Korea Kaskazini.

Hatua hiyo inakuja kufuatia agizo la Umoja wa Mataifa (UN) kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya taifa hilo kwa sababu ya jaribio lake la hivi karibuni la makombora ya masafa marefu.

Kufuatia jaribio hilo, hali ya wasiwasi imeendelea kutanda hasa nchini Marekani ambako majaribio kadhaa ya mwanzo yalielekezewa huko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!