Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Nyasi bandia zapata msahama wa Kodi
Michezo

Nyasi bandia zapata msahama wa Kodi

Spread the love

 

Waziri wa Fedha na Mipangango Mwigulu Nchemba amesema kuwa katika bajeti ya mwaka 2021/22 watasamehe ongezeko la kodi la thamani (VAT) kwa nyasi bandia kwa ajili ya marekebisho kwenye viwanja vibovu ili kukuza mchezo wa soka. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mwigulu amesema hay oleo bungeni tarehe 1o Juni, 2021 wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Katika eneo hilo Waziri Mwigulu amesema kuwa viwanja vingi vya michezo nchini ni vibovu kiasi cha kupelekea baadhi ya timu kama Yanga kutopata matokeo katika michezo ya mikoani.

“Viwanja vyetu vingi nchini ni vibovu na vinasababisha timu bora kama Yanga ikienda mikoani inashindwa kupata matokeo.” Alisema Mwigulu

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Aidha Waziri huyo aliongezea kuwa msamaha huo kwa kodi ya ongezeko la thamani kwa nyasi hizo zitausisha kwa viwanja vya mpira vilivyopo kwenye majiji.

“Napendekeza kusamehe kodi la ongezeko la thamani kwa nyasi za bandia, kwa ajili ya viwanja vya mpira vilivyopo kwenye Majiji na msahama huo utahusisha ridhaa kutoka kwenye Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).” Aliongezea Mwigulu

Serikali imeamua kuchukua hatua hiyo, kwa ajili ya kuendeleza michezo nchini, kwa kuwa na miundombinu bora kwenye sekta hiyo, ambapo kilikuwa kilio cha wadau kwa muda mrefu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!