Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nyalandu ainanga Chadema
Habari za Siasa

Nyalandu ainanga Chadema

Lazaro Nyalandu aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema kanda ya kati akihutubia mkutano mkuu wa CCM mara baada ya kurejea kwenye chama hiko.
Spread the love

 

SIKU mbili baada ya kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lazaro Nyalandu, amesema chama hicho tawala ni imara kuliko Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Nyalandu ambaye aliwahi kuwa mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati, amesema alipohamia Chadema, ndio alipojua kwamba CCM ni imara zaidi, hivyo hakuwa na budi kurejea.

“…lakini ni kweli, nilikwenda upinzani na baada ya kufika huko nikabaini CCM ni chama madhubutu na ndiyo maana nimeamua nimerejea,” amesema Nyalandu ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii wakati wa Utawala wa Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete.

Nyalandu ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, tarehe 3 Mei 2021, katika mahojiano maalum na kipindi cha Clouds360 cha Clouds Televisheni.

Mwanasiasa huyo alikuwa akijibu swali la kilichomtoa CCM kwenda Chadema kisha kurejea CCM ni ‘tumbo lake?’ amesema, “ningeondoka Chadema na kwenda NCCR-Mageuzi au TLP hiyo ingekuwa kutangatanga.”

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

Alipoulizwa ataikumbuka kwa lipi Chadema? amesema “wanachadema wengi ni watu wazuri sana, wanashauku kubwa, ukitaka kujua uzuri ambao wanawazidi CCM, itisha tu mkutano, watakuja wengi sana, kutoka maeneo mbalimbali.

“Lakini CCM, kimejaaliwa mifumo, itifaki ya chama, kuchaguana na kupokezana vijiti,” amesema Nyalandu, aliyedumu Chadema kwa siku 1,278

Pia, amekumbushia alivyoshambuliwa mitandaoni, mara baada ya yeye kwenda kushiriki maziko Chato, mkoani Geita ya Hayati Rais John Pombe Magufuli.

Tundu Lissu (kushoto) akijadiliana jambo na Lazaro Nyalandu

Amesema, baadhi ya wana Chadema walimshambulia ikiwa ni tofauti na alivyokwenda kumtembelea Nairobi nchini Kenya, Tundu Lissu, Makamu mwenyekiti wa Chadema-Bara, baada ya kushambuliwa.

“Nilipokwenda Chato kuzika, nilipata mashambulizi si kutoka CCM bali kutoka Chadema.”

“Lakini Lissu alipopata matatizo, nilikwenda kumwona, sikupata mashambulizi kutoka CCM au kiongozi yoyote, ndiyo maana nasema, kule wimbo hauimbiki,” amesema Nyalandu

Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana tarehe 7 Septemba 2017, katika makazi yake Area D, jijini Dodoma akitoka kuhudhuria mkutano wa Bunge.

Mwanasiasa huyo alijiunga na Chadema tarehe 30 Oktoba 2017, ambapo tarehe 30 Aprili 30, katika mkutano mkuu maalum wa CCM, mbele ya mwenyekiti wake mpya, Rais Samia Suluhu Hassan, alirejea ‘nyumbani.’

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!