Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko NSSF kukusanya Sh. trilioni 1.3 kwa mwaka
Habari Mchanganyiko

NSSF kukusanya Sh. trilioni 1.3 kwa mwaka

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara (kulia), akiangalia michoro ya nyumba
Spread the love

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linatarajia kukusanya kiasi cha Sh.trilioni 1.3 kwa mwaka wa fedha 2018/2019, anaadika Christina Haule.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Profesa Godias Kahyarara amesema hayo wakati akifungua mkutano wa Wakaguzi na Wafanyakazi waliopo kwenye kurugenzi ya uendeshaji kutoka  kanda ya mashariki uliofanyika mjini hapa Morogoro.

Kahyarara amesema shirika limeamua kufanya mkutano huo ili kutathmini mambo yatakayofanyika na kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa kufuatia mikoa ya kanda hiyo kuwa na uwezo wa kukusanya asilimia 60 ya mapato yote ya NSSF.

Amesema katika mwaka wa fedha 2016/17, kupitia mikoa hiyo waliweza kukusanya na kufikia kiasi cha makusanyo ya asilimia 64

“Kwa taifa tumeweka malengo ya makusanyo, na tumeweza kukusanya jumla ya Sh. bilioni  60 kwa miezi minane mfululizo kwa mwaka 2016 na kwa mwezi juni pekee tumeweza kukusanya kiasi cha Sh. bilioni  70.2” amesema

Aidha,  amesema kwa kutumia fedha hizo wanaweza kuimarisha malipo ya wanachama na pia kuingiza katika ufufuaji wa viwanda hasa kwenye suala zima la kilimo na kumuunga mkono Rais Magufuli.
Amesema tayari wameshatumia kiasi cha Sh. bilioni  8.71 kwa ajili ya kufufua viwanda kikiwemo kiwanda cha kutengeneza chaki Mufindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!