MWENYEKITI wa Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amepata tuzo kama mtetezi kijana chipukizi wa haki za binadamu (wanafunzi) Tanzania, tuzo aliyopewa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Nondo amesema kuwa tuzo hiyo kwake imekuwa na maana kubwa na kuweza kuinua hari mpya ya kuzidi kuwatetea wanafunzi katika haki zao katika masuala mbalimbali nchini na kudai tuzo hiyo imezidi kumuimarisha zaidi na kutokana tamaa na changamoto mbalimbali anazopitia katika kutetea haki za wanafunzi.
“Kwanza namshukuru Mwenyezimungu kwa kunipa Afya njema, pia wazazi wangu na viongozi wenzangu wa TSNP na watanzania wote kwa ujumla kwa faraja zao na matumaini yao kwangu. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mtandao wa THRDC kwa kutambua mchango wetu TSNP kwa kunizawadia tuzo kama mtetezi kijana chipukizi wa haki za binadamu (wanafunzi) Tanzania nimefarijika saana,” amesema Nondo.
Nondo amesema kuwa kwa kushirikiana na baadhi ya taasisi za serikali na taasisi hizo zimekuwa zikipokea na kusikia na kufanyia kazi baadhi ya mambo ambayo wamekuwa wakiyasemea.
Leave a comment