Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Nondo aibua kikwazo mikopo Chuo Kikuu
ElimuTangulizi

Nondo aibua kikwazo mikopo Chuo Kikuu

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Nchini (TSNP), Abdul Nondo amekitaja kikwazo kingine kwenye mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu ni Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini Rita. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Nondo akizungumza na MwanaHALISI Online amesema kuwa Rita wamekuwa kikwazo kwa mikopo ya wanafunzi kutokana na kuchelewesha kuhakiki taarifa za vyeti vya kuzaliwa za wanafunzi.

Amesema kuchelewa kupitia na kuhakiki taarifa za wanafunzi  kunawanyima fursa ya kupata mikopo kutokana muda kuisha na kwamba dirisha la kuomba mikopo linafungwa Tarehe 15 Mwezi huu.

“Sisi kama Mtandao wa wanafunzi tumeiandikia barua Bodi ya Mikopo kuiomba waongeze muda wa kuomba mikopo kutokana na kuhofia wanafunzi wengi watakosa mikopo kutokana na ucheleweshwaji wa uhakika wa vyeti unaofanywa na  Rita,” amesema Nondo.

Amewatoa hofu wanafunzi waliomba mikopo kuwa hoja ya TSNP ina maslahi kwao hivyo itasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

error: Content is protected !!