Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nondo aachiwa kwa dhamana Iringa
Habari za SiasaTangulizi

Nondo aachiwa kwa dhamana Iringa

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ameachiwa kwa dhamana leo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nondo ameachiwa baada ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia kutoa maamuzi kuwa dhamana ipo wazi na mtuhumiwa huyo kutimiza masharti ya dhamana.

Masharti ya dhamana ni kudhaminiwa na watu wawili ambao ni wakazi wa Iringa, huku mmoja awe mfanyakazi wa serikali, na wanatakiwa waweke bondi ya Sh. 5 milioni sambamba na kuwa na mali isiyohamishika, ambayo Nondo ameyatimiza na kupata dhamana.

Kesi imehairishwa mpaka Aprili 4, 2018 itakapotajwa tena mahakamani hapo.

Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili, la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma mjini Mafinga alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha Polisi Mafinga kuwa alitekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam na kupelekwa Kiwanda cha Pareto cha Mafinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!