MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ameachiwa kwa dhamana leo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Nondo ameachiwa baada ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia kutoa maamuzi kuwa dhamana ipo wazi na mtuhumiwa huyo kutimiza masharti ya dhamana.
Masharti ya dhamana ni kudhaminiwa na watu wawili ambao ni wakazi wa Iringa, huku mmoja awe mfanyakazi wa serikali, na wanatakiwa waweke bondi ya Sh. 5 milioni sambamba na kuwa na mali isiyohamishika, ambayo Nondo ameyatimiza na kupata dhamana.
Kesi imehairishwa mpaka Aprili 4, 2018 itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili, la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.
Shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma mjini Mafinga alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha Polisi Mafinga kuwa alitekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam na kupelekwa Kiwanda cha Pareto cha Mafinga.
Leave a comment