Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Nondo aachiwa huru kesi ya kujiteka
Habari MchanganyikoTangulizi

Nondo aachiwa huru kesi ya kujiteka

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Iringa leo imemkuta Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo hana hatia hivyo imemuachia huru. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Leo Novemba 5 mwaka 2018 Hakimu Liad Chamshama amemuachia huru Nondo baada ya upande wa Mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka yake mahakamani hapo.

Nondo alishitakiwa kwa kesi ya msingi ya kudanganya kuwa alitekwa, na kutoa taarifa za uongo, aliyoyatenda Machi 7, 2018.

Ushahidi wa Jamhuri

Upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi wake mahakamani hapo uliopelekea kumtia hatiani Nondo pamoja na ushahidi wa ofisa upelelezi wa makosa ya mitandao ambaye pia ni shahidi namba tano, koplo Abdulkadir ambaye alidai mahakamani hapo kuwa Nondo alikuwa akiwasiliana na Mange Kimambe Mtanzania anayeishia Marekani.

Koplo Abdukadir alidai kuwa alipokuwa akiifanyia uchunguzi simu ya Nondo alinasa mawasiliano yake na Mange Kimambe ya tarehe 25 Februari mwaka huu ambapo alieeleza“Ujumbe huo pia ulisema, amepata tetesi kuwa anatafutwa na watu wasiojulikana na kushauriwa asitembee peke yake kwa sababu ana hatihati ya kutekwa,” alidai koplo Abdulkadir.

Pia aliieleza mahakama hiyo kuwa Nondo alituma ujumbe saa 9:09 mchana siku ya tukio kwa kutumia simu ya mkononi kupitia mtandao wa Whatsap kwenda ka Paul Kisabo akiwa Ubungo uliosomeka “am at risk” .

Shahidi huyo alidai alikuta namba tatu za simu ambazo hazikupokewa katika simu ya Nondo ambazo zilipigwa kati ya saa nane mchana hadi 3:45 usiku.

Shahidi namba mbili koplo John alisema alimpokea mshtakiwa huyo katika Kituo cha Polisi Mafinga na kuandikisha maelezo yake.Koplo huyo alisema baada ya kuchukua maelezo hayo alibaini kuwa Nondo hakutekwa kama upelelezi wa koplo Abdulkadri ulivyobaini na hivyo waliamua kuripoti suala hilo katika uongozi wa juu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!