BENKI ya NMB nchini Tanzania ni miongoni mwa taasisi zilizoshiriki sherehe za Mei Mosi kitaifa jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu
Sherehe hizo zimefanyika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma na kuhudhuriwa na wafanyakazi mbalimbali ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Wafanyakazi wa NMB wamepita mbele ya jukwaa waliokaa viongozi mbalimbali akiwemo Rais Samia wakiwa wamebeba banki lililokuwa na ujumbe uliosomeka ‘Huduma bora kwa Wateja wetu ndiyo Utamaduni wetu.’
Leave a comment