Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB yaahidi kuendelea kutoa mikopo wawekezaji nishati nchini
Habari Mchanganyiko

NMB yaahidi kuendelea kutoa mikopo wawekezaji nishati nchini

Spread the love

BENKI ya NMB imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kutoa mikopo kwa wadau katika mnyororo wa thamani wa sekta ya nishati nchini kwa lengo  la  kusaidia ukuaji wa sekta hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akichangia mada ya “Umuhimu wa upatikanaji wa fedha na haki katika mamlaka” wakati wa Kongamano la Nishati lililofanyika jijini Dar es Salaam jana, Alfred Shao, Afisa Mkuu wa Wateja wa Jumla Benki ya NMB, alisema benki hiyo ina bidhaa nyingi za kifedha mahususi kusaidia wawekezaji watarajiwa katika sekta ya nishati chini.

Shao alisema benki hiyo ikiwa ni mshauri wa uwekezaji aliyeidhinishwa pia inatoa huduma za ushauri kwa wateja na pia wakati mwingine husaidia kutafuta mitaji kwa makampuni mapya.

“Sisi kama benki tunaelewa kuwa uwekezaji katika sekta ya nishati  unhitaji mitaji mikubwa. Tuna fedha za kutosha kutoa mikopo kwa wadau  kwenye sekta ya nishati.  Kwa sasa tunaweza kutoa mkopo wa mpaka bilioni 310 kwa mkopaji mmoja,” aliseme Shao.

Alisema benki hiyo pia imejenga ushirikiano mzuri na mashirika ya kifedha ya kimataifa kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Shirika la Kimataifa la Fedha (IFC) miongoni mwa wengine wanaopendelea hati fungani za kijani.

“Tulifanikiwa kutoa Hati Fungani Maaluum ‘NMB Jasiri Bond’ mwaka huu ambayo ilikuwa na mwitikio mzurim sana tunatarajia kutoa hati fungani ya kijani inayolenga sekta ya nishati jadidifu,” alisema.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Biashara na Uwekezaji, Exaud Kigahe wakati wa hafla hiyo alisema Serikali inatarajia kutumia fursa kwenye maeneo ambayo hayajatumika hasa katika nishati jadidifu yaani renewable energy na kusisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kufanya kazi na sekta binafsi katika kukuza sekta hiyo.

Alisema Serikali tayari imeanza utekelezaji wa mkakati wa kuboresha mazingiraya kufanya biashara nchini Tanzania huku akisisitiza dhamira ya Serikali ya kupunguza urasimu usio wa lazima miongoni mwa taasisi zake.

“Kwa nchi yetu haipo kwenye kiwango kizuri cha mazingira ya kufanya biashara . Tumepiga hatua kubwa kuweka mazingira mazuri ya biashara kama sehemu ya juhudi zetu za kuvutia wawekezaji zaidi nchini na hii itatusaidia kuongeza ushindani,” alisisitiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!