Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Njaa yaweka rehani ubunge wa Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Njaa yaweka rehani ubunge wa Zitto

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT na mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge pekee wa chama hicho ametangaza kujiuzulu ubunge wake iwapo serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), itathibitisha kuwa akiba ya chakula inayofikia tani milioni 1.5, anaandika Charles William.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini ametoa msimamo wa kujiuzu kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Facebook na Twitter.

“Serikali ya CCM ikinionesha tani 1.5 milioni za chakula ambazo inataka kusambaza, najiuzulu Ubunge mara moja. Narudia, mpaka Oktoba 2016 kulikuwa na nafaka tani 90,400 tu kwenye maghala yote ya NFRA.

“Tunashukuru kuwa Hivi sasa ajenda ya tishio la njaa inapata majawabu na matamko. Ndio wajibu wa vyama vya siasa. Kuibua masuala muhimu kwa nchi yetu,” ameandika Zitto.

Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imekuwa ikisisitiza kuwa taifa halijakumbwa na njaa na hakuna chakula cha msaada ambacho serikali itakipeleka kwa wananchi, bali wananchi wafanye kazi kwa bidii ili kujipatia kipato halali.

Hata hivyo, katika baadhi ya maeneo ya nchi, zimeripotiwa taarifa za kuwepo kwa uhaba wa chakula unaotokana na ukame kiasi cha kusababisha vifo vya mifugo kwa kukosa malisho.

Jana Waziri Mkuu Majaliwa Kassim aliwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa kuna akiba ya chakula inayofikia tani 1.5 milioni ambazo tayari wameruhusu zisambazwe katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili kuuzwa katika maeneo mbalimbali na kudhibiti kupanda kwa bei.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!