Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari Nitazindua miradi ya Chato mwenyewe: Rais Samia
Habari

Nitazindua miradi ya Chato mwenyewe: Rais Samia

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amesema ataizindua mwenyewe miradi yote inayotekelezwa Wilayani Chato mkoani Geita kama ambavyo angefanya mtangulizi wake Hayati Dk. John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Rais Samia ameyasema hayo leo Alhamis tarehe 17 2022 katika maadhimisho ya kumbukizi ya mwaka mmoja tangu kuondoka kwa kiongozi huyo wa Serikali ya awamu ya tano.

“Kwa hapa Chato naomba niwahakikishie kwamba miradi yote tuliyopanga na ambayo tumeshaanza kuitekeleza itakamilika nafahamu pia ujenzi wa kivuko cha Chato Hapa Kazi Tu, kimeshakamilika kwa asilimia 100 na kimegharimu Sh 3.1 bilioni, vilevile ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato umefikia asilimia 95 kwa gharama ya Sh 58.9 bilioni.”

“Stendi mpya ya Chato iliyogharimu Sh 13 bilioni imefikia asilimia 90 na mabasi madogo yameshaanza kuingia naomba niwaahidi wana Chato, miradi yoye ikikamilika nitakuja kuizindua mwenyewe kama ambavyo angefanya Dk. Magufuli angekuwepo,” amesema Rais Samia

Aidha amesema “nimearifiwa Hospitali ya Rufaa ya kanda inayojengwa kwa Sh 34 bilioni, unaendelea vizuri na baadhi ya huduma zimeanza kutolewa. Niwahakikishie tutakamilisha yote hata ile midogo ambayo sijaitaja hapa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!