Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu NIT inavyohamasisha wanawake kusoma Sayansi
ElimuHabari Mchanganyiko

NIT inavyohamasisha wanawake kusoma Sayansi

Spread the love

IKIWA imebaki siku moja Dunia kuadhimisha siku ya wanawake duniani kesho Jumanne 8 Machi 2022, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimetoa hamasa kwa wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi kwa kuwa wao wana mchango kwenye maendeleo ya jamii. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Akizungumza katika semina ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa kike, leo Jumatatu, tarehe 7 Machi 2022 chuoni hapo Mabibo jijini Dar es Salaam, Profesa Zacharia Mganilwa, Mkuu wa chuo hicho amesema, wanawake wakiwa mstari wa mbele kwenye masomo ya sayansi jamii itapata maendeleo haraka.

Amesema mfumo wa maisha wa jamii wanawake wamekuwa na majukumu mengi yanayoanzia nyumbani, kazini mpaka kwenye jamii.

Ameutaja mfano wa kukosekana ugunduzi wa mashine ya kupika ugali kwa sababu wanasanyasi wengi ni wanaume.

Amesema chuo hicho wiki mbili zilizopita kimetoa timu maalum ya hamasa iliyokwenda mikoa ya Kusini (Lindi na Mtwara) iliyokwenda kwenye shule za mikoa hiyo kuhamasisha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi.

“Tunaye mwanafunz wa kike hapa aliyepata daraja la juu la kwanza la hesabu ambaye tukimpatia ajira hapa anapokwenda kuhamasisha wanafunzi wengine wanaona mfano nzuri, na watahamisika kuona kuwa mtaalamu wa Sayansi ni Mwanamke” amesema Profesa Mganilwa.

Amesema chuo hicho kina mifano mingi yenye kutoa hamasa kwa wanafunzi wa kike kusoma sayansi, mathalan mkuu wa idara ya kompyuta na Mkuu Idara ya Hesabati na Sayansi ya jamii ni wanawake.

Profesa Mganilwa ametoa wito kwa wanafunzi wa kike kuyachukulia masomo ya sayansi kuwa ni kama masomo mengine.

Amesema 50\50 isiishie kwenye siasa mpaka kwenye masomo na mambo mengine yahusiayo maendeleo ya Sayansi.

Kuhusu semina hiyo, amesema imeandaliwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo wanawake kukabiliana na changamoto wanazokumbana nazo kazini, nyumbani na katika jamii.

Dk. Zainab Mshani, Naibu Mkuu Fedha Mipango na Utawala wa chuo cha NIT amesema chuo hicho kimefanya semina kwa ajili ya wanawake kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.

Amesema kwenye semina hiyo kutawasiliswa mada mbalimbali ikiwemo matatizo ya afya ya akili na masuala ya kiuchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!