ABDALLAH Shaibu (Ninja) amerejea tena ndani ya Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya La Garaxy inayoshiriki ligi kuu nchini Marekani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezaji huyo amesaini mkataba huo mapema hii leo kwenye makao makuu ya klabu hiyo chini ya makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Frederick Mwakalebela na kaimu katibu mkuu wa klabu hiyo Patrick Simon.
Beki huyo hapo awali alijiunga na Yanga 2017 akitokea Zanzibar kwa mkataba wa miaka miwili, na kufanikiwa kucheza Yanga kwa mafanikio makubwa na mwisho wa msimu alijiunga na klabu ya La Garaxy na baadae kupelekwa kwa mkopo kwenye timu ya MFK Vyskov.
Yanga kwa sasa inaendelea kuimalisha kikosi chake ambapo mpaka sasa imeshasajili jumla ya wachezaji watano ambao ni Zawadi Mauya, Bakari Mwamnyeto, Wazir Junior, Yassin Mustapha na Ninja.
NINJA KARIBU KWA WANANCHI UPIGE SOCCER