Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Neymar, wenzake wakumbwa na corona
Kimataifa

Neymar, wenzake wakumbwa na corona

Spread the love

NEYMAR de Santos, mshambuliaji wa timu ya Paris Saint-Germain (PSG) ya nchini Ufaransa na wachezaji watatu wa timu hiyo, amekutwa na virusi vya corona. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Licha ya kalbu hiyo kutotaja majina ya wachezaji wengine waliokumbwa na ugonjwa huo sambamba na Neymar, taarifa kutoka klabuni hapo zinaeleza wanaotajwa kukumbwa na corona ni pamoja na Angel Di Maria (32) na Leandro Paredes (26).

PSG kwenye Ligi Kuu ya taifa hilo, ni mabingwa watetezi ambapo kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya, wameshika nafasi ya pili.

Taarifa za wachezaji hao kukumbwa na corona, zimethibitishwa na taarifa ya klabu hiyo iliyowekwa kwenye mitandao yao ya kijamii.

Neymar na wenzake, kwa sasa wamewekwa karantini kwa siku 14 wakiendelea na matibabu. Ligi Kuu nchini humo tayari imeanza kuchezwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!