Monday , 29 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa New Zealand kufanya tukio la kihistoria leo
Kimataifa

New Zealand kufanya tukio la kihistoria leo

Spread the love

KUSHAMBULIWA na kuua wa kwa Waiumini wa Dini ya Kiislam msikitini kumeibua mambo mengi nchini New Zealand ikiwa ni pamoja na kuimarisha mshikamano wa dini zote. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Leo Ijumaa tarehe 22 Machi 2019, Televisheni na Redio ndani ya taifa hilo zitatangaza moja kwa moja adhana, huku wanawake wengi wakitarajia kuvaa vazi la kiislamu la Hijab kama ishara ya kuonesha uzalendo na umoja wa taifa hilo.

Waziri Mkuu wa New Zealand, Jacinda Adern amesema siku ya Ijumaa ambayo ni siku ya ibada kwa waumini wa kiislamu, taifa hilo litakuwa kimya kwa muda wa dakika mbili, wakati adhana ikiadhiniwa kitaifa kupitia televisheni pamoja na redio ya taifa hilo.

Adern amesema, tukio hilo ni ishara ya kuonesha umoja wa taifa hilo, kufuatia tukio baya na la kusikitisha la shambulizi la risasi lililotokea katika misikiti miwili ya Al Noor na Linwood iliyoko katika mji wa Christchurch, lililotokea Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya waislamu 50.

Taarifa zinaeleza kuwa, Arden ataungana na waombolezaji wengine karibu na msikiti wa Al-Noor ambao ni miongoni mwa miskiti iliyokumbwa na shambulio la risasi Ijumaa iliyopita.

Wanawake wengi nchini New Zealand wametakiwa kuvaa Hijab kuonesha ishara ya kupinga tukio hilo.

Hadi sasa raia wa Australia, Brenton Tarrant amefunguliwa shtaka la mauwaji akiwa mshukiwa mkuu katika tukio hilo. Vile vile, Bunge la New Zealand  limepiga marufuku uuzaji wa silaha za moto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!