Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria
Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Benjamini Netanyau, Waziri Mkuu wa Israel
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha sehemu muhimu ya mipango yenye utata ya kurekebisha mfumo wa sheria ambao umefanya hali ya utulivu kurejea nchini huko. Anaripoti Eliabu Kanyika, DSJ kwa msaada wa mtandao … (endelea).

Aliyasema hayo jana Jumatatu usiku tarehe 27 Machi 2023 kuwa atasitisha sheria ili kuzuia mpasuko kati ya watu. Lakini haijulikani ni nini kucheleweshwa kutafanikisha zaidi ya kujipa muda hadi utulivu urejee.

Pia katika matukio ambayo hayajawahi kushuhudiwa, chama kikuu cha wafanyakazi nchini humo kiliitisha mgomo, na Waisrael waliitazama huduma kote zikisitishwa. Uwanja wa ndege, maduka, hospitali na benki kote huduma zilisimamishwa.

Hatua hiyo iliyoratibiwa ilibunuwa kumrudisha Netanyahu kutoka kwenye ukingo wa kusukuma mbele mageuzi mwishoni mwa wiki hii.

Sambamba na hilo ilifuatia maandamano makali baada ya kumfuta kazi waziri wake wa ulinzi ambaye alikuwa amezungumza kupinga mipango hiyo. Kiongozi wa Upinzani Yair Lapid aliuita “mgogoro mkubwa zaidi katika historia ya nchi”.

Serikali ya mrengo wa kulia zaidi ya Israel kuwahi kutokea, inatafuta kuchukua udhibiti madhubuti juu ya kamati inayoteua majaji. Marekebisho hayo yangeipa bunge mamlaka ya kubatilisha maamuzi ya Mahakama ya juu kwa wingi wa kimsingi na yangefanya iwe vigumu kutangaza waziri mkuu asiyefaa kushika wadhifa huo na kuwaondoa mamlakani

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!