Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Netanyau ang’olewa baada ya kuongoza Israel miaka 12
Kimataifa

Netanyau ang’olewa baada ya kuongoza Israel miaka 12

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyau, ameng’olewa katika wadhifa huo alioushikilia kwa miaka 12, baada ya Bunge kupiga kura za kumuondoa madarakani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Netanyau aliingia madarakani kwa mara ya kwanza 1996 hadi 1999, kisha 2009 alichaguliwa tena kuwa Waziri Mkuu wa Israel, nafasi aliyohudumu hadi jana Jumapili, alipong’olewa.

Jana tarehe 13 Juni 2021, Netanyau aliondolewa madarakani kwa kura za ndiyo 60 kati ya 120 zilizopigwa, ambapo 59 zilipigwa kwa ajili ya kupinga mwanasiasa huyo mkongwe Israel kuondolewa madarakani, huku moja ikiharibika.

Naftali Bennett, Waziri Mkuu wa Israel

Kufuatia hatua hiyo, Bunge hilo lilimchagua mzalendo mwenye mrengo wa kulia, Naftali Bennett, kuwa Waziri Mkuu wa Israel, ambaye ataongoza umoja wa vyama vya siasa nchini humo.

Kwa mujibu wa makubaliano ya vyama hivyo, Bennett, amabaye ni Kiongozi wa Chama cha Yamina, atashikilia wadhifa huo hadi Septemba 2023, kisha Yair Lapid, atachukua madaraka na kuiongoza Israel kwa miaka miwili.

Kwa sasa Netanyau anabaki kuwa Mkuu wa Chama cha Mrengo wa Kulia cha Likud, ambacho kwa sasa kinakuwa chama cha upinzani nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!