Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Netanyahu: Israel imeingia kwenye vita virefu na vigumu, zaidi ya 900 wameuawa
KimataifaTangulizi

Netanyahu: Israel imeingia kwenye vita virefu na vigumu, zaidi ya 900 wameuawa

Spread the love

 

TAKRIBANI Waisraeli 900 wameripotiwa kuwawa na 100 wengine kutekwa nyara katika mashambulizi yaliyoendeshwa na vikosi vya wanamgambo wa Hamas ndani ya Israel. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyonukuliwa na vyombo vya habari ya serikali ya Israel, zinaeleza kuwa Waisraeli hao wameuawa tangu kuanza kwa mashambulizi hayo, jana Jumamosi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zaidi ya watu 100 wametekwa nyara na wengine zaidi ya 2,000 wamejeruhiwa.

Hata hivyo, wanamgambo wa Hamas, wamesema leo kwamba watatoa idadi kamili ya wanajeshi na raia wa Israel wanaowashikilia mateka ndani ya saa chache zijazo.

Aidha, Hamas wamesama wataendeleza kile wanachokiita, “kulipiza kisasi kwa uvamizi wa Israel.”

Mapigano kati ya wanajeshi wa Israel na wanamgambo wa Kipalestina yaliyoanza mwishoni mwa wiki, yamesababisha umwagikaji mkubwa wa damu.

Katika eneo la Gaza, takriban watu 370 wameuawa kufuatia mashambulizi ya anga ya Israel, kwa mujibu wa maafisa wa Palestina.

Vikosi vya Israel vinadai vimeweza kuwaokoa raia wa nchi hiyo waliotekwa na wanamgambo wa Kipalestina kutoka Gaza na kurejesha udhibiti wa baadhi ya maeneo yaliyotekwa.

Jeshi lilisema kuwa wanajeshi walikuwa wamekomboa maeneo 22 kusini mwa Israel lakini bado wanapambana katika maeneo mengine manane.

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amenukuliwa akisema, taifa lake linaingia kwenye “vita virefu na vigumu.”

Ameonya Hamas, ambayo inatawala Gaza, kwamba maficho yake yatageuzwa kuwa “vifusi.”

Lakini kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh, anasema kuwa wanatazamia “ushindi mkubwa” katika vita hivyo.

Wizara ya Afya huko Gaza – ambayo inasimamiwa na Hamas – inasema watu 313 wameuawa katika mashambulizi ya anga ya Israel.

Afisa mmoja aliniambia zaidi ya nusu yao ni raia. Idadi hiyo pia inajumuisha zaidi ya watoto 20 na wanawake sita, mmoja wao akiwa mjamzito.

Israel inasema inalenga nyumba za makamanda wa Hamas, lakini raia pia wametumbukizwa katikati ya mashambulizi hayo.

Kumekuwa na wito kwa Wapalestina kufika hospitalini na kuchangia damu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataka jamii inayohoji mafisadi

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo juu ya uboreshaji dira...

Habari za SiasaTangulizi

Kapinga: Kukatika kwa umeme siyo hujuma

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali ipo kazini...

error: Content is protected !!