BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza kuondoa utaratibu wa kutangaza shule 10 bora na watahiniwa 10 bora kwa matokeo ya mitihani mbalimbali kwa kuwa utaratibu huo hauna tija. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 29 Januari 2023 jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athuman Amas, amesema wameondoa utaratibu wa kutangaza shule 10 bora na watahiniwa 10 bora kwa sababu hauna tija.
“Tulizoea kusikia shule bora, mtahiniwa bora, wasichana wawagaragaza wanaume, tulizoea kwa muda mrefu kusikia hayo… sasa tuondokane na mazoea.
“Ukigundua jambo unalolifanya halina tija hauna haja ya kuendelea nalo, unamtaja mtu ameongoza na kumlinganisha na watu ambao hawakusoma katika mazingira yaliyofanana sio sahihi,” amesema.
Amesema kama kuna shule ilikuwa inasubiri itangazwe kuwa kwenye ‘Top 10’ hiyo haipo kwa sababu huwezi kutangaza shule moja wakati shule zipo zaidi ya 11,000.
“Kwanza kutangaza shule ya kwanza huenda tulikuwa tunakufanyia marketing (kukutangaza kibiashara), tumeona haina tija” amesema.
Leave a comment