Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko NECTA yapiga ‘stop’ kutangaza shule, watahiwani 10 bora
Habari Mchanganyiko

NECTA yapiga ‘stop’ kutangaza shule, watahiwani 10 bora

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athumani Amasi
Spread the love

BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza kuondoa utaratibu wa kutangaza shule 10 bora na watahiniwa 10 bora kwa matokeo ya mitihani mbalimbali kwa kuwa utaratibu huo hauna tija. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 29 Januari 2023 jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athuman Amas, amesema wameondoa utaratibu wa kutangaza shule 10 bora na watahiniwa 10 bora kwa sababu hauna tija.

“Tulizoea kusikia shule bora, mtahiniwa bora, wasichana wawagaragaza wanaume, tulizoea kwa muda mrefu kusikia hayo… sasa tuondokane na mazoea.

“Ukigundua jambo unalolifanya halina tija hauna haja ya kuendelea nalo, unamtaja mtu ameongoza na kumlinganisha na watu ambao hawakusoma katika mazingira yaliyofanana sio sahihi,” amesema.

Amesema kama kuna shule ilikuwa inasubiri itangazwe kuwa kwenye ‘Top 10’ hiyo haipo kwa sababu huwezi kutangaza shule moja wakati shule zipo zaidi ya 11,000.

“Kwanza kutangaza shule ya kwanza huenda tulikuwa tunakufanyia marketing (kukutangaza kibiashara), tumeona haina tija” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!