Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo ‘Ndoa’ ya Simba, Sven yavunjika
Michezo

‘Ndoa’ ya Simba, Sven yavunjika

Kocha Mkuu wa Simba Sven Vandenbroeck
Spread the love

MABIGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba imetangaza kuachana na kocha wake mkuu, Sven Vandenbroeck. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Simba imetangaza kuachana na Sven Alhamisi usiku tarehe 7 Januari 2021 kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na timu hiyo, ambayo haikueleza sababu ya uamuzi huo.

Sven ameachana na Simba baada ya kuifikisha hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuitoa FC Platinum ya Zimbambwe kwa magoli 4-0 kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa Uwanja wa Benjamim Mkapa Dar es Salam.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki mbili zilizopita, Harare nchini Zimbabwe, Simba ilifungwa goli 1-0.

Sven ameondoka Simba akiwa ameichia mafanikio msimu uliopita kwa kutetea kombe la ligi kuu, kutwaa kombe la shirikisho na ngao ya jamii.

Taarifa hiyo ya Simba imesema, kocha msaidizi, Suleiman Matola ataiongoza timu hiyo hadi atakapopatikana kocha mwingine.

Simba kwa sasa iko visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya mapinduzi ambapo leo Ijumaa saa 10:15 jioni itashika dimbani kucheza na Chipukizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!