Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo ‘Ndoa’ ya Simba, Sven yavunjika
Michezo

‘Ndoa’ ya Simba, Sven yavunjika

Kocha Mkuu wa Simba Sven Vandenbroeck
Spread the love

MABIGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba imetangaza kuachana na kocha wake mkuu, Sven Vandenbroeck. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Simba imetangaza kuachana na Sven Alhamisi usiku tarehe 7 Januari 2021 kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na timu hiyo, ambayo haikueleza sababu ya uamuzi huo.

Sven ameachana na Simba baada ya kuifikisha hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuitoa FC Platinum ya Zimbambwe kwa magoli 4-0 kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa Uwanja wa Benjamim Mkapa Dar es Salam.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki mbili zilizopita, Harare nchini Zimbabwe, Simba ilifungwa goli 1-0.

Sven ameondoka Simba akiwa ameichia mafanikio msimu uliopita kwa kutetea kombe la ligi kuu, kutwaa kombe la shirikisho na ngao ya jamii.

Taarifa hiyo ya Simba imesema, kocha msaidizi, Suleiman Matola ataiongoza timu hiyo hadi atakapopatikana kocha mwingine.

Simba kwa sasa iko visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya mapinduzi ambapo leo Ijumaa saa 10:15 jioni itashika dimbani kucheza na Chipukizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!