Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Ndoa ya Ndayilagije na TFF yafikia mwisho
Michezo

Ndoa ya Ndayilagije na TFF yafikia mwisho

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF
Spread the love

 

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imevunja rasmi mkataba na aliyekuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Etienne Ngayilagije baada ya kukubaliana kwa pande zote mbili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Ettiene alikuwa anakinoa kikosi cha Taifa Stars baada ya kuchukua mikoba kutoka kwa Emannuel Amunike aliyetimuliwa kwa kufanya vibaya kwenye michuano ya kombe la Mataifa Afrika (AFCON) 2019 yaliyofanyika nchini Misri.

Taarifa kutoka TFF iliyotolewa muda mfupi hii leo tarehe 11 Februari 2021, imeleza kuwa pande zote mbili zimefikia makubaliano hayo baada ya kikao cha pamoja.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa mchakato wa kumapata mbadala wa Ndayilagije utaanza hivi karibuni ili kurithi nafasi yake.

Pengine kufanya vibaya kwenye michuano ya kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) kwa Taifa Stars ndio sababu kubwa ya kuondolewa kwa kocha huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!