Saturday , 3 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Ndege ya Ethiopia yapata ajali, 157 wahofiwa kufariki
KimataifaTangulizi

Ndege ya Ethiopia yapata ajali, 157 wahofiwa kufariki

Spread the love

NDEGE ya kampuni ya Ethiopia aina ya Boeing 737 iliyokuwa ikisafiri kutoka Adis Ababa kuelekea Nairobi imeanguka Jumapili asubuhi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndege hiyo iliyokuwa imebeba abiria 149 na wafanyakazi wa ndege nane, ilipata ajali hiyo kuda mchache baada ya kuruka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole, Adis Ababa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika hilo la ndege inasema kuwa ajali hiyo imetokea maeneo ya Bishoftu nje kidogo ya jiji la Adis Ababa.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa ndege hiyo yenye usajili ET-AVJ iliruka uwanjani hapo leo saa 2:36 lakini ilipoteza mawasiliano saa 2:44 na baadavya muda kugundulika imepata ajali.

Pia taarifa hiyo haijathibitisha ni watu wangapi wamefariki kufuatia ajali hiyo na imewataka ndugu wa abiria waliosafiri na ndege hiyo wawe watulivu mpaka hapo watakapotoa taarifa rasmi.

Ofisi ya waziri Mkuu wa Ethiopia, Abey Ahmed imethibitisha kutokea kwa ajali hiuo na kutoa salamu za rambirambi kwa familia za walio wapoteza wapendwa wao katika jali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!