Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR-Mageuzi yapinga matokeo uchaguzi, yataka meza ya majadiliano
Habari za Siasa

NCCR-Mageuzi yapinga matokeo uchaguzi, yataka meza ya majadiliano

Spread the love

CHAMA cha NCCR-Mageuzi nchini Tanzania, kimetangaza kutoyatambua matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumatano ya tarehe 28 Oktoba 2020 kwa madai miongozo mwa kanuni za uchaguzi huo zilikiukwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Msimamo huo umetolewa leo Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma wa NCCR Mageuzi, Edward Simbeye kwa niaba ya mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia.

“Uchaguzi ni mchakato, kanuni na miongozo ya uchaguzi vyote hivi vimekiukwa na vinapelekea matokeo kutokuwa halali ya kinachoitwa uchaguzi. Kwa sasa ni sawa na hakuna aliyeshinda wala aliyeshindwa,” amesema Sembeye.

Akizungumzia ukiukwaji wa baadhi ya kanuni na miongozo uliojitokeza katika uchaguzi huo, Sembeye amesema, kuna baadhi ya maeneo mawakala wa NCCR-Mageuzi walizuiwa kuingia katika vituo ya kupigia kura.

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi

“Ukienda Vunjo, robo tatu ya mawakala hawakuruhusiwa kuingia kwenye vituo.
Mimi na wewe tujiulize kama Mbatia anayesema Tanzania kuhusu muungano na ushirikiano anafanyiwa figisu vipi kwa mtu ambaye hana jina,” amehoji Sembeye.

“Ukienda kituo cha Kawe, mgombea wetu wa ubunge hata kura yake ya majumuisho haipo kuna sifuri. Ukiangalia uchaguzi ni mchakato kwa kuwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho ulikuwa wa makandokando na kusababisha matokeo yake ya uchaguzi kutokuwa halali,” amesema Sembeye.

Kufuatia dosari hizo, NCCR-Mageuzi kimeomba meza ya majadiliano ili kupata muafaka wa sintofahamu ya matokeo ya uchaguzi huo kwa lengo la kurudisha imani ya Watanzania na Taifa lao.

“Nchi inakwenda kupasuka. Turudini kwenye meza ya majadiliano NCCR tuko tayari kupata mufaka wa kitaifa. Miaka yote tukekuwa mstari wa mbele kutangaza amani na kuunganisha nchi, bado tuna nafasi ya kurudisha imani ya Watanzania na nchi yao hasa katika kipindi kilichopo, chuki imepitiliza tunahitaji muafaka wa kitaifa,” amesema Sembeye.

NCCR-Mageuzi kimekuwa chama cha nne kutangaza kupinga matokeo hayo kikitanguliwa na vyama vya Chadema, CUF na ACT-Wazalendo.

Katika uchaguzi huo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejizolea viti vingine vya ubunge, udiwani na kuendelea kushinda urais ambapo mgombea wake, Dk. John Pombe Magufuli aliibuka mshindi akiwashinda wenzake 15.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!