Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR-Mageuzi yagomea wabunge viti maalumu
Habari za Siasa

NCCR-Mageuzi yagomea wabunge viti maalumu

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi
Spread the love

CHAMA cha NCCR-Mageuzi nchini Tanzania kimesema, hakiko tayari kupokea nafasi za ubunge wa viti maalumu kwani kitakuwa kinachochea machafuko kwenye jamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Msimamo huo umetolewa leo Alhamisi tarehe 12 Novemba 2020 na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia wakati anazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mbatia ametoa wito huo alipoulizwa na wanahabari kama chama chake kiko tayari kupokea nafasi za ubunge viti maalumu.

Amesema, NCCR-Mageuzi hakitakubali kwa kuwa itakuwa ni kinyume na sheria inayoeleza, chama kitakachofikisha asilimia tano ya kura zote za wabunge kitakuwa na nafasi ya kupata wabunge wa viti maalum.

“Kwamba sisi NCCR- Mageuzi tutapewa viti ni suala lingine na tusingependa kuwa sehemu ya machafuko, wakati tunazungumzia muafaka halafu watupe viti maalumu kinyume na sheria, hatutakubali sababu sisi ni waasisi wa mageuzi Tanzania na tusingependa mageuzi ya demokrasia yakiukwe,” amesema Mbatia.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

NCCR-Mageuzi kimeungana na baadhi ya vyama vingine vya siasa vya upinzani nchini Tanzania vilivyotangaza kugoma kupokea nafasi hizo, hatua ambayo ni muendelezo wa kutoyatambua matokeo ya uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 yaliyozalisha nafasi hizo.

Vyama vilivyotangaza kutotambua matokeo hayo kwa madai kwamba mchakato wa uchaguzi ulikiuka sheria na kanuni za uchaguzi, ni ACT-Wazalendo na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (CUF).

Matokeo hayo yaliyotangwa na Tume ya Taufa ya Uchaguzi Tanzania (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yalikipa ushindi Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Urais, ubunge, uwakilishi na udiwani.

Hadi sasa chama kilichokidhi matakwa ya kisheria kupewa nafasi hizo ni Chadema, ambacho mpaka sasa kimeweka msimamo wa kutokubali uteuzi wa wabunge viti maalumu.

Kufuatia Chadema kugomea nafasi hizo, Mbatia amesema kama mamlaka husika zitagawa nafasi hizo kwa vyama vingine  itakuwa ni kinyume.

“Viti maalumu vya ubunge vinapatikana kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na sheria hii inaeleza bayana chama kinachopata asilimia tano ya kura za wabunge ndicho chenye nafasi kupata viti maalumu kama kuna chama kimekataa huwezi kufanya kienyeji kuwapa chama kingine huko ni kutafuta machafuko katika jamii,” amesema Mbatia.

Mbatia ameishauri NEC, ZEC na Bunge kufuata sheria katika utoaji nafasi za Ubunge Viti Maalumu ili kuepusha migogoro katika jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!