CHAMA cha siasa cha upinzani nchini Tanzania, NCCR-Mageuzi, kimemwomba Rais wa Taifa hilo, Samia Suluhu Hassan, kuufikilia upya uamuzi wake kuhusu suala la katiba mpya na mikutano ya hadhara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
NCCR-Mageuzi kimesema, suala la Katiba mpya ni takwa la wananchi linalopaswa kutekelezwa huku mikutano ya hadhara ipo kwa mujibu wa sheria hivyo inapaswa kuruhusiwa.
Hayo yamesemwa na Edward Simbeye, Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma wa NCCR-Mageuzi, alipofanya mahojiano maalum na MwanaHALISI TV kuhusu siku 100 za utawala wa Rais Samia.
Rais Samia aliingia madarakani tarehe 19 Machi 2021, baada ya aliyekuwa Rais wa taifa hilo, John Pombe Magufuli, kufariki dunia.
Mapema wiki hii, Rais Samia akizungumza na wahariri na waandishi wa habari Ikulu ya Dar es Salaam kuhusu siku 100, alisema suala la katiba mpya na mikutano ya hadhara, isubiri kwanza hadi aisimamishe nchi kiuchumi.
Fuatilia mahojiano kati ya MwanaHALISI TV na Simbeye.
Leave a comment