Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Nauli mabasi ya mwendokasi kupanda Januari 16
Habari MchanganyikoTangulizi

Nauli mabasi ya mwendokasi kupanda Januari 16

Spread the love

 

WAKALA wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), umetangaza nauli mpya kwa watumiaji wa mabasi yaendayo haraka, zitakazoanza kutumika kuanzia tarehe 16 Januari 2023. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Nauli hizo mpya ambazo zimeongezeka kwa wastani wa Sh. 100, zimetangazwa leo tarehe 14 Januari 2023 na DART kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Taarifa ya DART imeeleza kuwa, nauli hizo mpya zimeidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA).

Nauli ya Kimara hadi Kivukoni, Gerezani na Morocco imeongezeka kutoka Sh. 650 hadi 750, wakati Gerezani hadi Muhimbili ikiwa Sh. 750 badala ya 650. Nauli ya Kutoka Kimara hadi Mbezi imepanda kutoka Sh. 400 hadi 500. Kimara hadi Kibaha (Sh. 650 hadi 700), Kimara hadi Mloganzila (Sh. 650 hadi 700).

Aidha, nauli kwa wanafunzi haijapanda, imebaki Sh. 200.

MwanaHALISI Online imeutafuta uongozi wa DART kwa njia ya simu, kwa ajili ya kupata sababu za ongezeko hilo, bila mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!