Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa NASA wajiondoa kwenye uchaguzi Kenya
Kimataifa

NASA wajiondoa kwenye uchaguzi Kenya

Raila Odinga, aliyekuwa mgombea wa Muungano wa NASA
Spread the love

MUUNGANO wa vyama vya Nasa umetangaza kujitoa rasmi katika uchaguzi mkuu wa Kenya uliopangwa kufanyika tarehe 26 Oktoba mwaka huu, anaandika Mwandishi Wetu.

Uamuzi wa kujiondoa katika uchaguzi huo umetangazwa leo na Raila Odinga, mgombea urais wa muu ngano wa Nasa, kwa madai kuwa uchaguzi unaotarajia kufanyika mwishoni mwa Oktoba mwaka huu si halali.

Odinga amekishutumu chama cha Jubilee na Rais Uhuru Kenyatta kwa kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya sheria za uchaguzi katika kipindi hiki amvbacho kampeni zinaendelea na kusema kuwa hatua hiyo inalenga kukibeba chama hicho katika utangazaji wa matokeo.

Wakati hayo yakiendelea, Rais Kenyatta ameendelea na mikutano yake ya kampeni katika kaunti ya Voi ambapo amewataka Wakenya wasiyumbishwe na Odinga na chama chake na badala yake waendelee kujiandaa na uchaguzi mkuu, Oktoba 26 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!