Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nape Nnauye apata ajali leo asubuhi Liwale
Habari za Siasa

Nape Nnauye apata ajali leo asubuhi Liwale

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa jimbo la Mtama,  amepata ajali asubuhi ya  leo tarehe 24 Septemba 2018  akiwa safarini kuelekea wilaya ya Liwale mkoani Lindi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, Nape pamoja na wengine waliokuwemo ndani ya gari hawajapata madhara makubwa ya kiafya.

Nape alikuwa njiani akielekea Liwale kwa ajili ya kushiriki ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally. Vile vile, alitarajiwa kushiriki kikao cha Kamati Kuu ya Siasa ya Mkoa wa Lindi.

Hali ya Mbunge huyo, inaendelea vizuri na ameandika katika ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Twitter, akimshukuru Mungu pamoja  na wanakijiji cha Kibutuka kwa msaada wao wa baada ya kupata ajali hiyo.

Nape aliandika: “Mwenyezi Mungu kaniokoa na ajali mbaya leo asubuhi, wakati natoka Mtama kuelekea kwenye kikao cha chama Liwale. Namshukuru sana Mwenyezi Mungu. Nawashukuru sana wananchi wa kijiji cha Kibutuka, wamenisaidia sana, Upendo wenu umenigusa sana! Familia,Viongozi na marafiki nawashukuru sana!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!