Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Nape Nnauye apata ajali leo asubuhi Liwale
Habari za Siasa

Nape Nnauye apata ajali leo asubuhi Liwale

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa jimbo la Mtama,  amepata ajali asubuhi ya  leo tarehe 24 Septemba 2018  akiwa safarini kuelekea wilaya ya Liwale mkoani Lindi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, Nape pamoja na wengine waliokuwemo ndani ya gari hawajapata madhara makubwa ya kiafya.

Nape alikuwa njiani akielekea Liwale kwa ajili ya kushiriki ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally. Vile vile, alitarajiwa kushiriki kikao cha Kamati Kuu ya Siasa ya Mkoa wa Lindi.

Hali ya Mbunge huyo, inaendelea vizuri na ameandika katika ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Twitter, akimshukuru Mungu pamoja  na wanakijiji cha Kibutuka kwa msaada wao wa baada ya kupata ajali hiyo.

Nape aliandika: “Mwenyezi Mungu kaniokoa na ajali mbaya leo asubuhi, wakati natoka Mtama kuelekea kwenye kikao cha chama Liwale. Namshukuru sana Mwenyezi Mungu. Nawashukuru sana wananchi wa kijiji cha Kibutuka, wamenisaidia sana, Upendo wenu umenigusa sana! Familia,Viongozi na marafiki nawashukuru sana!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!