Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Nani kuibuka mshindi Liberia leo?
Kimataifa

Nani kuibuka mshindi Liberia leo?

George Weah, Mshindi wa Urais
Spread the love

WANANCHI nchini Liberia leo wanapiga kura kumchagua mrithi wa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa rais barani Afrika na mshindi wa tuzo la amani la Nobel, Ellen Johnson Sirleaf.

Aliyekuwa mcheza kandanda nyota George Weah, na makamu wa rais Joseph Boakai ndiyo wagombea wenye nguvu katika kinyang’anyiro

Liberia ni nchi iliyobuniwa na watumwa walioachiliwa huru kutoka Marekani karne ya 19, haijakuwa na mabadiliko ya amani ya madaraka kwa kipindi cha miaka 73.

Sirleaf aliwashauri watu kupiga kura kwa amani kwenye taifa hilo ambalo bado linajijenga kutoka kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 14.

“Kura yako inakuhusu wewe na familia yako, sio chama wala kabila,” alisema Sirleaf wakati akihutubia taifa. Jumla ya wagombea 20 wa urais wanawania urais kumrithi Sirleaf.

Rais wa sasa mwenye umri wa miaka 78 anaondoka madarakani baada kuongoza kwa mihula miwili.

Aliingia madarakani mwaka 2006 baada ya mtangulizi wake Charles Taylor, kulazimishwa kuondoka madarakani na waasi mwaka 2003.

Taylor kwa sasa anatumikia kifungo cha miaka 50 jela nchini Uingereza kwa makosa yanayohusu uhalifu wa kivita na mzozo katika nchi jirani ya Sierra Leone.

Weah mwenye umri wa miaka 51, amemteua mke wa zamani wa Taylor Jewel Howard, kama mgombea mwenza.

Sirleaf ameshindwa kumfanyia kampeni Boakai na kuzua uvumi kuwa wawili hao huenda wametofautiana.
Karibu watu milioni 2.2 wamejiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi huo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!