Monday , 29 May 2023
Home Kitengo Michezo Nane waingia kinyang’anyiro tuzo mchezaji bora Epl
Michezo

Nane waingia kinyang’anyiro tuzo mchezaji bora Epl

Harry Kane
Spread the love

 

 WACHEZAJI nane kutoka klabu tofauti ndani ya Ligi Kuu nchini England wameingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo ya mchezaji bora wa Ligi hiyo kwenye msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

 Ligi hiyo ilimalizika wiki mbili zilizopita na klabu ya Manchester City kutwaa taji hilo mara baada ya kuwa na msimu mzuri na wamafanikio chini ya kocha Pep Guardiolla.

Mohamed Salah

Waliongia kwenye kinyang’anyiro hiko ni kiungo mshambuliaji wa klabu ya Manchester City Kelvin De Bruyne, Kiungo wa Manchester United Bruno Fernandes, mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane na Jack Glealish kutoka Astorn Villa.

Wengine ni Ruben Dias mlinzi wa kati wa kikosi cha Manchester City, mshambuliaji wa timu ya Liverpool Mohammed Salah, Tomas Soucek kutoka Westham na Mason Maount wa klabu ya Chelsea.

Bruno Fernandes kiungo wa Manchester United

Wachezaji hao nane walichaguliwa mara baada ya kuwa na msimu mzuri kwenye klabu zao na wadau na mshindi atachaguliwa kwa kupigiwa kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!