Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Tangulizi Namna Kibonde alivyoanza safari ya kifo chake
Tangulizi

Namna Kibonde alivyoanza safari ya kifo chake

Spread the love

SAFARI ya mwisho ya Ephrahim Kibonde, mtangazaji na Mahiri wa  Clouds FM aliyekuwa akitangaza kipindi cha Jahazi,  ilishika kasi siku ya mazishi ya Ruge Mutahaba yaliyofanyika katika Kijiji  cha Kiziru, Bukoba mkoani Kagera. Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).

Akiwa msibani hapo, Kibonde ndiye aliyekuwa mtangazaji wa shughuli za mazishi zilizokuwa zikiendelea na hapo mwisho  wake ulianza kudhihiri.

Mmoja wa watangazaji wa Clouds aliyeomba kutoandikwa jina lake hapa amesema, yapo mambo yaliyotokea kwenye msiba wa Ruge yanayoendana na mwisho wa uhai wake.

Mwandishi huyo anasimulia, Kibonde alianza kujisikia vibaya wakati wa shughuli za mazishi ya mfanyakazi mwenzie,  rafiki yake wa muda mrefu Ruge.

Kibonde alianza kuishiwa nguvu ambapo dada wa marehemu Ruge alimsaidia. Dada huyo pamoja na watu waliokuwepo karibu wakamsaidia kumuingiza ndani na kuanza kumpepea.

Alipoana hali inazidi kuwa mbaya, dada huyo alimwita  Dk.Isack Maro ambaye ni mtangazaji wa kipindi cha Njia Panda na Afya Cheki kwa ajili ya huduma ya kwanza.

Dk.Maro alimpatia huduma ya kwanza na kumpeleka Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kagera.

Kesho yake (Jumanne) ilibidi wenzake waliokuwa wana ratiba ya kusafiri na ya kurudi Dar es Salaam baada ya kumaliza maziko, walilazimika wamuache Bukoba ili aendelee na matibabu zaidi.

Akiwa anaendelea na matibabu hospitalini hapo, hali yake ilizidi kuwa mbaya, wakafanya uamuzi wa kumuhamishia Hospitali ya Uhuru jijini Mwanza, wakati akipelekwa hospitali ya Bugando leo asubuhi kwa matibabu zaidi umauti ukamkuta.

Taarifa za msiba huo tayari zimedhibitishwa na uongozi wa Clouds Media pamoja na John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa  Mwanza.

“Mtangazaji wa Clouds FM Kibonde amefariki dunia hapa Mwanza, alianza kusumbuliwa na presha alipokuwa Bukoba kwenye msiba wa marehemu Ruge Mutahaba na kuhamishiwa  Mwanza,” amesema Mongella.

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari za SiasaTangulizi

⁩ Samia aridhia Chongolo kujiuluzu

Spread the loveMwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano ameridhia...

Habari MchanganyikoTangulizi

13 wafariki dunia ajali ya basi likigonga treni Singida

Spread the loveJUMLA ya watu 13 wakiwamo wanawake sita na wanaume saba...

Habari MchanganyikoTangulizi

33 wanusurika ajali ya ndege Mikumi

Spread the loveJUMLA ya abiria 30, marubani wawili na mhudumu mmoja wamenusurika...

error: Content is protected !!