Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Namaingo wazindua mradi mpya Msolwa
Habari Mchanganyiko

Namaingo wazindua mradi mpya Msolwa

Biubwa Ibrahimu, Mkurugenzi wa Namaingo
Spread the love

JUHUDI za Taasisi ya Namaingo Business Agents (NBA), imezindua mradi Shamba Mji Msolwa wilayani Mkuranga, Pwani ikiwa ni mwendelezo wa kuinua uchumi wa nchi kupitia kilimo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mradi wa Shamba Mji utakuwa na hekari 7,000 ambapo utahusisha mashamba na makazi pamoja na huduma za kijamii ikiwa pamoja na soko la kuuza mazao yatakayotokana na mazao ya shamba hilo.

Biubwa Ibrahimu, Mkurugenzi wa Namaingo amesema uzinduzi mashamba hayo yatakuwa kichecheo kikubwa cha kunyanyua uchumi wa wakulima, wakazi wanaozunguka maeneo ya mashamba na nchi kwa ujumla.

Amesema kupitia mradi huo wakulima watapata fulsa ya kupata ushauri wa kupanda mazao kwa ubora ikiwa pamoja na kugeuza kutoka kilimo cha chakula na kulima kilimo cha biashara.

Diwani wa Kata ya Mbezi, Rashid Selungwi, amesema kuwa wananchi wa eneo hilo wamefurahia ujio wa mradi huo utakaowaletea maendeleo makubwa kwani hiyo ni moja ya fulsa kwa wakazi wa Msolwa.

Mwakilishi wa Wazee wa kijiji cha Msolwa, Ali Kitasa ameubariki mradi huo na kuwaombea dua walulima watakaojishughulisha na mradi huo kwani anaamini kuwa mafanikio yao yatawagusa wakazi wa eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!