JUHUDI za Taasisi ya Namaingo Business Agents (NBA), imezindua mradi Shamba Mji Msolwa wilayani Mkuranga, Pwani ikiwa ni mwendelezo wa kuinua uchumi wa nchi kupitia kilimo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Mradi wa Shamba Mji utakuwa na hekari 7,000 ambapo utahusisha mashamba na makazi pamoja na huduma za kijamii ikiwa pamoja na soko la kuuza mazao yatakayotokana na mazao ya shamba hilo.
Biubwa Ibrahimu, Mkurugenzi wa Namaingo amesema uzinduzi mashamba hayo yatakuwa kichecheo kikubwa cha kunyanyua uchumi wa wakulima, wakazi wanaozunguka maeneo ya mashamba na nchi kwa ujumla.
Amesema kupitia mradi huo wakulima watapata fulsa ya kupata ushauri wa kupanda mazao kwa ubora ikiwa pamoja na kugeuza kutoka kilimo cha chakula na kulima kilimo cha biashara.
Diwani wa Kata ya Mbezi, Rashid Selungwi, amesema kuwa wananchi wa eneo hilo wamefurahia ujio wa mradi huo utakaowaletea maendeleo makubwa kwani hiyo ni moja ya fulsa kwa wakazi wa Msolwa.
Mwakilishi wa Wazee wa kijiji cha Msolwa, Ali Kitasa ameubariki mradi huo na kuwaombea dua walulima watakaojishughulisha na mradi huo kwani anaamini kuwa mafanikio yao yatawagusa wakazi wa eneo hilo.
Leave a comment