Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Naibu Spika awapongeza wabunge Mwambe, Rose kuoana, awapa darasa
Tangulizi

Naibu Spika awapongeza wabunge Mwambe, Rose kuoana, awapa darasa

Wabunge Cecil Mwamba na Rose Tweve
Spread the love

 

NAIBU Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu leo tarehe 27 Mei, 2022 amewapongeza wabunge Cecil Mwamba na Rose Tweve wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kufunga ndoa hivi karibuni na kuongeza kuwa ni neema kwa Bunge hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Pia Zungu ambaye ni Mbunge wa Ilala (CCM) ametoa darasa kwa wabunge wanaume kwamba wasio mwanamke mzuri pekee bali waoe mwanamke mwema vivyo hivyo wanawake wasiolewe na mwanamume mzuri pekee bali waolewe na mwanaume mwema.

Zungu ametoa kauli hiyo leo bungeni jijini Dodoma baada ya kipindi cha maswali na majibu ambapo pamoja na mambo mengine amesema jana tarehe 26 Mei, 2022 alimuona Rose Tweve (Mbunge Viti Maalumu Iringa) ndani Bunge.

Naibu Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu

“Kwa kweli lazima niwapongeze kwa wabunge wawili kuoana humu ndani ni neema kwetu.

“Sidhani kama na nyie mligundua kuna vitu vinapitapita lakini wamefanya heshima na wamefanya staha mpaka kufikia kuunganisha roho zao pamoja,” amesema na kuongeza;

“Kwa hiyo ninawapongeza sana… usioe mke mzuri, oa mke mwema kwa sababu uzuri unakwisha wema hauishi na usitake kuolewa na mwanaume mzuri, olewa na mwanaume mwema kwa sababu uzuri unakuisha wema hauishi,” amesema.

Amesema jana hakumuona Cecil Mwambe ambaye ni Mbunge wa Ndanda (CCM) na leo wote hawapo hivyo inawezekana wanafuatilia cheti cha ndoa yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!