NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azan Zungu, ameonya wabunge wanaokiuka kanuni za utoaji taarifa bungeni na kwamba kufanya hivyo itakuwa ni kosa la utovu mkubwa wa nidhamu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Zungu ameyasema hayo leo tarehe 13 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma mara baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu.
Amesema kuelekea mjadala wa bajeti kuu Mbunge yeyote atakeshindwa kufuata kanunia ya kutoa taarifa atakuwa amefanya, “kosa la utovu mkubwa wa nidhamu ikiwa itapuuza maamuzi ya Spika au Mwenyekiti wa Bunge” kwa mujibu wa kanuni ya 84 (1) (a).
“Kuanzia mjadala wa bajeti kuu kakutakuwapo tena na taarifa za mchezo humu ndani na mmeona hivi karibuni wabunge wanalalamika mnaingilia flow zao za uchangiaji. Kwahiyo nawaomba mfuate mwongozo wa kiti kwani taarifa zimekuwa nyingi hazina maana bali za kupoteza muda na kumtoa mbunge kwenye reli,” amesema Zungu.
Leave a comment