
MSANII wa muziki wa bongo fleva Nandela Charles Mfinanga maarufu Nandy leo Jumamosi tarehe 4 Septemba 2021 anahitimisha kilele cha tamasha lake ‘Nandy Festival. Anaripoti Matilda Peter… (endelea)
Tamasha hilo lililoanzia Mkoa wa Kigoma tarehe 6 Juni 2021, litahitimishwa katika viwanja vya Posta, Kijitonyama mkoani Dar es Salaam na kuwakutanisha wasanii mbalimbali nchini humo.
Miongoni mwa mikoa aliyopita; ni Mwanza, Arusha, Mtwara, Dodoma na Zanzibar ambako kila alikopita alikonga nyonyo za mashabiki zake akiwa na wasanii kama Alikiba, Lina Sanga, Babalevo, Mr blue, Fid q na Whozu.
https://www.youtube.com/watch?v=YxnxkbO7Kug
Wasanii mbalimbali wa watahitimisha kilele hicho leo Jumapili akiwemo Willy Paul kutokea nchini Kenya.
Kutoka Tanzania, watakaopanda jukwaani; ni Baba levo, Young lunya, Juma Nature, Rosa ree, Linah Sanga, Whozu, Dullah Makabila, Sholomwamba, Weusi, Saraphina, Mabantu na Juma Jux.
More Stories
Apple Music yasherehekea mafanikio ya Bara la afrika
Mastaa wa muziki Afrika waachia African Lullabies Part 2 kwa kishindo
Rayvanny ‘aifuta’ Wasafi