Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu NACTVET yafungua dirisha la udahili
Elimu

NACTVET yafungua dirisha la udahili

Spread the love

 

BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limefungua dirisha la udahili wa mkupuo wa mwezi Machi kwa mwaka wa masomo wa 2023/24 kuanzia tarehe 16 Januari 2023. Anaripoti Selemani Msuya, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo imesema kwamba vyuo vyote vinaruhusiwa kudahili wanafunzi katika mkupuo huu, isipokuwa vyuo vinavyotoa mafunzo ya Afya na Sayansi Shirikishi kwa Tanzania Bara.

Taarifa hiyo imesema vyuo vya Afya na Sayansi shirikishi vilivyopo Tanzania Visiwani vyenye uwezo wa kudahili katika mkupuo huo vinaruhusiwa ikiwa vitakidhi vigezo.

Katika taarifa yake hiyo, NACTVET limevielekeza vyuo vinavyohitaji kudahili wanafunzi kwa mkupuo huu kutuma maombi yao kabla ya tarehe 27 Januari 2023 kwa kujaza fomu inayoonesha uwezo wa chuo kuendesha mafunzo na kuiwasilisha katika ofisi za Kanda za Baraza ambapo chuo husika kipo.

“Uwezo huo ni pamoja na kuwa na miundombinu na walimu wa kutosha kutoa mafunzo katika mikupuo miwili kwa mwaka (Machi na Septemba)” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Baraza hilo limesema kwamba fomu ya maombi inapatikana katika tovuti ya Baraza hilo www.nacte.go.tz kwa kubofya fomu ya maombi ya udahili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!