Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Michezo NACTE: Vyuo ndiyo wanachelewesha udahili elimu ya juu
Michezo

NACTE: Vyuo ndiyo wanachelewesha udahili elimu ya juu

Twaha A. Twaha, Mkuu wa Kitengo cha Udahili NACTE (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Spread the love

BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevitaka vyuo na taasisi za elimu kutoa matokeo ya wahitimu wao mapema kwa ajili ya kuwarahisishia kupata Namba ya Uhakiki wa Tuzo (AVN) itakayowawezesha kujiunga na elimu ya juu kwa wakati husika. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 24 Agosti, 2018 na Twaha A. Twaha, Mkuu wa Kitengo cha Udahili NACTE wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Twaha amesema kuwa, baadhi ya wahitimu wamekuwa wakikwama kupata AVN kwa wakati husika kutokana na vyuo na au taasisi zao kutowasilisha mapema matokeo yao halisi NACTE.

“Kumekuwepo na malalamiko ya baadhi ya wahitimu wa ngazi ya stashahada na hasa waliomaliza masomo yao kwa mwaka wa masomo 2017/2018 hadi mwezi Julai, 2018.

Baadhi ya wahitimu hao mara tu baada ya kumaliza mitihani yao na kupatiwa matokeo ya awali wamekuwa wakiomba AVN kwa kuambatanisha hati za matokeo ya awali wakati vyuo na taasisi husika hazijawasilisha NAVTE matokeo halisi yaliyoidhinishwa na mamlaka husika,” amesema Twaha na kuongeza.

“Na pia uhakiki wa matokeo yao haujakamilika kwenye mfumo wa uhakiki wa Tuzo wa Baraza. Ifahamike kwamba hakuna mhitimu wa ngazi ya diploma anayeweza kujiunga na elimu ya juu bila kuwa na AVN.

“Huu ni utaratibu uliowekwa na baraza ili kurahisisha utambuzi wa tuzo za elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

error: Content is protected !!