Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mzozo Kosovo na Serbia waongeza hatari ya kuzuka vita
Kimataifa

Mzozo Kosovo na Serbia waongeza hatari ya kuzuka vita

Spread the love

JESHI la Serbia linasema liko katika “kiwango cha juu zaidi cha utayari wa mapigano” baada ya wiki kadhaa za mvutano unaoongezeka kati ya Serbia na Kosovo. Yanaripoti Mashirka ya Kiamtaifa … (endelea)

Rais Aleksandar Vucic anasema “atachukua hatua zote kulinda watu wetu na kuhifadhi Serbia”.

Hata hivyo, serikali ya Pristina haijasema lolote kuhusu madai hayo. Lakini hapo awali imemshutumu Vucic kwa kucheza “michezo” ili kuchochea matatizo.

Umoja wa Ulaya umekuwa ukijaribu kupatanisha. Umoja huo wenye wanachama 27 unatoa wito wa “kuzuiliwa kwa kiwango cha juu zaidi na hatua za haraka”, na kwa viongozi wa Serbia na Kosovo “kuchangia kibinafsi suluhisho la kisiasa”.

Serbia inakataa kutambua Kosovo kama nchi huru. Kosovo, ambayo ina watu wengi wa kabila la Albania, ilijitenga na Serbia baada ya vita mwaka 1998-99.

Nato, ambayo ina wanajeshi wa kulinda amani huko Kosovo, imetoa wito kwa pande zote kuepuka uchochezi.

Umoja wa Ulaya umeonya kuwa hautavumilia mashambulizi dhidi ya polisi wa Umoja wa Ulaya au vitendo vya uhalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!