Tuesday , 23 April 2024
Habari za SiasaTangulizi

Mwingine apotea​

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo
Spread the love

ADUL Nondo, mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambaye alikuwa mstari wa mbele kupinga kitendo cha jeshi la Polisi kumpiga risasi, Akwiline Akwelina, amepotea katika mazingira ya kutatanisha. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).

Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na Nondo zinasema, kabla ya “kupotea” hewani, mwanafunzi huyo alijitoa kwenye makundi yote ya mtandao wa Whatsapp aliyokuwa amejiunga.

Nondo ambaye ni mwenyekiti wa TSNP, amekuwa mstari wa mbele kushinikiza serikali kufanya uchunguzi wa mauaji ya Akwiline.

Akwiline aliuawa kwa kupigwa risasi na jeshi la Polisi, tarehe 6 Februari mwaka huu, kwenye maeneo ya Mkwajuni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam, akiwa ndani ya basi ya daladala.

Akwiline alikuwa akitokea maeneo ya Mabibo kwenda Bagamoyo kwa mafunzo ya vitendo.

Habari zinasema, taarifa rasmi kwa umma zitatolewa kwa waandishi wa habari saa majira ya 9:30 alasiri kwenye ukumbi wa Kituo cha Sheria na Haki Za Binadamu LHRC.

Katika siku za karibuni, kumeibuka kundi kubwa la vitendo vya utekaji, utesaji na mauaji nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!