ADUL Nondo, mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambaye alikuwa mstari wa mbele kupinga kitendo cha jeshi la Polisi kumpiga risasi, Akwiline Akwelina, amepotea katika mazingira ya kutatanisha. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).
Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na Nondo zinasema, kabla ya “kupotea” hewani, mwanafunzi huyo alijitoa kwenye makundi yote ya mtandao wa Whatsapp aliyokuwa amejiunga.
Nondo ambaye ni mwenyekiti wa TSNP, amekuwa mstari wa mbele kushinikiza serikali kufanya uchunguzi wa mauaji ya Akwiline.
Akwiline aliuawa kwa kupigwa risasi na jeshi la Polisi, tarehe 6 Februari mwaka huu, kwenye maeneo ya Mkwajuni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam, akiwa ndani ya basi ya daladala.
Akwiline alikuwa akitokea maeneo ya Mabibo kwenda Bagamoyo kwa mafunzo ya vitendo.
Habari zinasema, taarifa rasmi kwa umma zitatolewa kwa waandishi wa habari saa majira ya 9:30 alasiri kwenye ukumbi wa Kituo cha Sheria na Haki Za Binadamu LHRC.
Katika siku za karibuni, kumeibuka kundi kubwa la vitendo vya utekaji, utesaji na mauaji nchini.
Leave a comment