Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Mwingine apona corona Tanzania
HabariTangulizi

Mwingine apona corona Tanzania

Spread the love

MPAKA sasa, watu watatu wawaliokuwa wakisumbuliwa na ugonjwa wa corona, wamepona. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea)

Taarifa iliyotolewa na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo tarehe 3 Aprili 2020, inaeleza kwamba mtu mmoja aliyekuwa na ugonjwa huo ameruhusiwa kuungana na familia yake baada ya kupona.

Mtu huyo anafanya idadi ya watu waliopona corona kufika watatu huku wengine 16 wakiendelea kupata matibabu. Kutokana na ugonjwa huyo, mto mmoja tayari ameripotiwa kufariki.

“Mgonjwa wa tatu aliyeambukizwa ugonjwa wa corona nchini, amepona na kuruhusiwa kurudi nyumbani. Mgonjwa  mwingine mmoja kipimo cha pili kimeonesha hana tena virusi vya corona  hivyo anasubiri kipimo cha mwisho kuthibitishwa kupona,” amesema Waziri Ummy.

Amesema, mmoja wa wagonjwa hao ni yule aliyekuwa amelazwa kwenye kituo maalumu ya tiba cha  Mkoa wa Kagera, na kwamba mpaka sasa mkoa huo hauna mgonjwa.

“Arusha tulikuwa na wagonjwa wawili, mmoja aliruhusiwa na mgonjwa mwingine majibu ya leo asubuhi yameonesha kuwa ni ‘negative,’ (hana maambukizi) hivyo tunasubiri kipimo kingine kimoja ili aweze kuruhusiwa,” amesema Waziri Ummy.

Pia amewakumbusha wananchi kukaa mita moja au zaidi kati ya mtu mmoja na mtu mmoja ili kuweza kuzuia maambukizi mapya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!