Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwina Kaduguda ateuliwa kumrithi Nkwabi Simba
Michezo

Mwina Kaduguda ateuliwa kumrithi Nkwabi Simba

Mwina Kaduguda
Spread the love

BODI ya Wakurugenzi ya Simba, imemteua Mwina Kaduguda kukaimu nafasi ya Mwenyekiti wa klabu akichukua nafasi iliyoachwa na Swed Nkwabi aliyejiuzuru wakati wakisubiri mchakato wa uchaguzi wa kuziba nafasi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Uteuzi huo wa Kaduguda unakuja baada ya klabu hiyo kukaa kwa miezi miwili bila ya Mwenyekiti toka kujiuzulu kwa Nkwabi Septemba, 14 mwaka huu, huku taarifa ya klabu hiyo ikisema kuwa mchakato wa uchaguzi wa kuziba nafasi hiyo utatangazwa hivi karibuni.

Kaduguda anakwenda kumrithi Nkwabi ambaye alijiuzulu miezi 10 baada ya kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika Novemba, 5, 2018 na kuwa mwakilishi wa wanachama katika bodi ya wakurugenzi baada ya kupitwa bila kupingwa.

Wakati huohuo, bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo imemteua Salum Abdallah kuwa makamu mwenyekiti wa bodi hiyo na uteuzi huo umeanza toka tarehe Novemba 19 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!