Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mwili wa Profesa Ndulu kuzikwa Dar leo
Habari

Mwili wa Profesa Ndulu kuzikwa Dar leo

Benno Ndulu, aliyekuwa Gavanna wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT)
Spread the love

 

MWILI wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu (71), unazikwa leo Alhamisi tarehe 25 Februari 2021, katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Anaripoti Matrida Peter…(endelea)

Profesa Ndulu, aliyekuwa Gavana kati ya mwaka 2008-2018, alifikwa na mauti tarehe 22 Februari 2021, katika Hospitali ya Regency, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Baadhi ya waombolezaji waliojitokeza kuuga mwili wa aliyekuwa Gavanna wa Benki Kuu, Prof. Benno Ndulu

Jana Jumatano, mwili wa Profesa Ndulu, aliyezaliwa tarehe 23 Januari 1950, ulilazwa nyumbani kwake, Mbweni, Dar es Salaam ambapo Ibada ya kumuombea na kumuaga, ilifanyika kwa ndugu, jamaa na marafiki.

Profesa Ndulu, aliwahi kuwa Naibu Gavana kati ya mwaka 2007-2008 na baadaye kuteuliwa na Rais wa wakati huo, Jakaya Kikwete kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania kuanzia 2008-2018

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

error: Content is protected !!